
Nafasi za kazi Udereva Nchini Qatar, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu kwa kushirikiana na mawakala wa ajira wakiwemo kampuni tanzu ya Global Solutions, inawatangazia Watanzania wenye sifa kuomba nafasi 800 za kazi ya udereva zilizotangazwa na kampuni ya MOWASALAT ya nchini Qatar kama ifuatavyo:
Nafasi za kazi Udereva Nchini Qatar

Maelezo ya Nafasi ya Kazi
- Nafasi: Dereva
- Kampuni: Mowasalat
- Nchi: Qatar
- Umri: Miaka 25 hadi 45
- Elimu: Awe amemaliza angalau kidato cha nne
Sifa za Waombaji
- Awe na uzoefu wa kuendesha magari kwa zaidi ya miaka 2
- Awe na uwezo wa kuwasiliana kwa lugha ya Kiingereza
- Wanaojua Kiarabu watapewa kipaumbele
Mshahara
Mshahara utalipwa kulingana na sera ya kampuni na sheria za nchi ya Qatar.
Matibabu
Gharama za matibabu kwa kipindi chote cha ajira zitalipwa na mwajiri.
Taarifa Muhimu 📝
- Mwajiri atagharamia visa na tiketi ya ndege
- Mwajiri atatoa malazi na chakula kipindi chote cha ajira
- Mwajiri atagharamia usafiri kutoka nyumbani hadi kazini
- Mwajiri atagharamia gharama za visa na tiketi ya kurudi baada ya mkataba kuisha
Aina ya Ajira: Mkataba
Leseni ya Udereva Inayotakiwa: Daraja C au E
Tangazo Limetolewa: Mei 9, 2025
Mwisho wa Kutuma Maombi: Mei 16, 2025
Waombaji wote watume wasifu wao (CV) kupitia:
International Career
📞 +255749639354, +255678203223
🌐 www.manpower.cgs.co.tz
📞 +255748883355, +255675899410
📧 [email protected]
📞 +255782821089, +255710882820
📧 [email protected]
📞 +255694521912
Baada ya kutuma maombi, hakikisha unasajili kwenye tovuti: https://jobs.kazi.go.tz
📞 +255784301987
Imetolewa na:
Katibu Mkuu
Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu
Be the first to comment